• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua ya Pepe |
Busokelo District Council
Busokelo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Usafishaji na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi na Zima moto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

BUSOKELO DC KUSAKA VIPAJI VYA MPIRA KWA VIJANA, YAHIMIZA UMUHIMU WA MICHEZO KATIKA MAENDELEO.

Imewekwa tarehe: February 12th, 2026

BUSOKELO DC KUSAKA VIPAJI VYA MPIRA KWA VIJANA, YAHIMIZA UMUHIMU WA MICHEZO KATIKA MAENDELEO.

Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo inatarajia kuzindua programu ya kusaka na kuibua vipaji vya mpira wa miguu kwa vijana wa wilaya hiyo, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha sekta ya michezo na kukuza vipaji vya vijana ngazi ya jamii.

Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Afisa Maendeleo ya Michezo wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo, Bw. Lewis Mwasekaga, amesema kuwa programu hiyo inatekelezwa kwa kushirikiana na Kocha Geofray Katepa, kocha wa zamani wa Mbeya City na Karonga United, kwa lengo la kutambua, kulea na kukuza vipaji vitakavyoiwakilisha Busokelo katika mashindano mbalimbali.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa, zoezi la kusaka vipaji litafanyika katika vituo mbalimbali kama ifuatavyo: Februari 21, 2026 katika Shule ya Sekondari Ntaba; Februari 22, 2026 katika Shule ya Msingi Lupata; Februari 28, 2026 katika Shule ya Msingi Kandete; na Machi 01, 2026 katika Shule ya Msingi Lwangwa. Zoezi litaanza saa 2:00 asubuhi katika kila kituo.

Bw. Mwasekaga amewahimiza wazazi na walezi kuwahamasisha watoto wao kushiriki katika majaribio hayo ili kuwapa fursa ya kutimiza ndoto zao kupitia michezo. Amesema michezo si burudani tu, bali ni nyenzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Michezo ina mchango mkubwa katika maisha ya vijana na jamii kwa ujumla. Kwanza, huimarisha afya ya mwili na akili kwa kupunguza magonjwa yasiyoambukiza na kuongeza nidhamu binafsi. Pili, hujenga maadili mema kama ushirikiano, uvumilivu, uongozi na kujituma.

Aidha, michezo hutoa ajira na kipato kwa vijana wenye vipaji, huku ikitangaza wilaya na taifa kwa ujumla kupitia mashindano ya kitaifa na kimataifa. Kupitia programu kama hii, Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo inalenga kuandaa kizazi chenye afya, nidhamu na uwezo wa kujiajiri au kuajiriwa kupitia sekta ya michezo.

uwekezaji katika michezo ni uwekezaji katika maendeleo ya vijana na ustawi wa jamii nzima.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA. December 09, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA AJIRA YA MKATABA October 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA AJIRA April 11, 2023
  • TANGAZO LA UKODISHAJI MAGHALA YA KUHIFADHIA KOKOA June 05, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BUSOKELO DC KUSAKA VIPAJI VYA MPIRA KWA VIJANA, YAHIMIZA UMUHIMU WA MICHEZO KATIKA MAENDELEO.

    February 12, 2026
  • CMT BUSOKELO YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, YAAGIZA MIRADI YOTE IKAMILIKE IFIKAPO 20/01/2026.

    January 15, 2026
  • SHILINGI BILIONI 32.9 ZAIDHINISHWA BAJETI YA HALMASHAURI MWAKA WA FEDHA 2026/2027.

    January 14, 2026
  • MIRADI YA MAENDELEO YENYE JUMLA YA THAMANI YA SHILINGI BILIONI 6.6 YAKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA BUSOKELO.

    October 10, 2025
  • Angalia zote

Video

Mkurugenzi atoa hamasa ya chakula kwa watoto mashuleni
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • Hati ya Mshahara
  • Orodha ya Madiwani
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Rais
  • Tovuti ya Mkoa wa Mbeya
  • Sekretarieti ya Ajira

Kipimo cha Wateja duniani

world map hits counter

Wateja waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Lwangwa, Tukuyu

    Anuani ya Posta: S. L. P. 2, Tukuyu

    Simu: +255 737 205 318

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@busokelodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2019 Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo. Haki zote zimehifadhiwa.