RC MBEYA ATOA MAAGIZO KWA HALMASHAURI KUSIMAMIA MIRADI NA KUONGEZA MAPATO.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Beno Malisa, amezitaka Timu za Wataalamu katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mbeya kuhakikisha zinafanya ziara za mara kwa mara za ukaguzi wa miradi ya maendeleo ili kufuatilia utekelezaji wake na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika maeneo yao.
Mhe. Malisa ametoa rai hiyo leo tarehe 19 Februari 2026 wakati akifungua kikao maalumu cha kupokea na kujadili Taarifa za Utekelezaji wa Shughuli mbalimbali za Serikali kutoka Halmashauri na Taasisi za Serikali kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2025/2026.
Katika kikao hicho, Mhe. Malisa amesisitiza kuwa usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo ni wajibu wa viongozi na wataalamu wa Halmashauri, akibainisha kuwa Serikali imeendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya, miundombinu ya barabara, maji na kilimo katika Mkoa wa Mbeya.

Ameeleza kuwa ni muhimu miradi hiyo kusimamiwa kwa weledi, kukamilika kwa wakati na kuwanufaisha wananchi kiuchumi na kijamii.
Aidha, amezitaka Halmashauri zote kuongeza juhudi katika ukusanyaji wa mapato ya ndani, na amesisitiza umuhimu wa kurejeshwa kwa wakati mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri kwa vikundi vya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu,.
Mhe.Malisa amesitiza kuhusu namna bora ya kutatua changamoto zinawakabili wakulima.
Kikao hicho kimehudhuriwa na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri zote saba za Mkoa wa Mbeya, Timu za Wataalamu wa Halmashauri, Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya pamoja na wataalamu kutoka taasisi mbalimbali za Serikali zikiwemo (TMA), (TFRA), (TPHPA), (TOSCI), (TARURA), (TANROADS), Electric Supply Company (TANESCO) (RUWASA).

Kwa ujumla, kikao hiki ni chachu ya kuimarisha uwajibikaji, kuongeza mapato fursa za kiuchumi kupitia biashara ,kilimo na miradi ya maendeleo inayotekelezwa ili kuleta matokeo chanya kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya kwa maendeleo endelevu.







Lwangwa, Tukuyu
Anuani ya Posta: S. L. P. 2, Tukuyu
Simu: +255 737 205 318
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@busokelodc.go.tz
Hakimiliki ©2019 Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo. Haki zote zimehifadhiwa.