KIDELI SASA BASI, CHANJO YA KUKU YA YAZINDULIWA RASMI BUSOKELO.
Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo imezindua rasmi kampeni ya utoaji chanjo ya kideli kwa ajili ya kuku,uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya ofisi ya Halmashauri na kuhudhuriwa na wataalamu wa mifugo pamoja na wafugaji leo 09 June,2025.
Akizungumza katika uzinduzi huo Kaimu wa Idara ya kilimo,Mifugo na Uvuvi Bw. Celestine Kimaro amesema kuwa zoezi hili ni la kitaifa na linafanyika Tanzania nzima, na chanjo hii ni mpango wa serikali wa miaka mitano kuanzia 2025 mpaka 2030.
Halmashauri ya Busokelo inatarajia kutoa chanjo kwa kuku 180,000 na wataalamu wa mifugo watapita kila kijiji kuhakikisha kuku wote wanapatawa chanjo hiyo.
Aidha, Daktari wa Mifugo wa Halmashauri amethibitisha kuwa chanjo inayotolewa ni kwa ajili ya kuzuia ugonjwa wa kideli ambao unasababishwa na virusi ambavyo huathiri kuku hasa kuku wadogo,ugonjwa huo unaambukizwa kwa njia ya hewa na dalili zake ni pamoja na kinyesi cha kijani,homa kali na kusababisha kifo mara moja endapo kuku hatapatiwa chanjo.
Sambamba na hilo mwakilishi wa Wafugaji Bw.Ally Kitogelo ameishukuru serikali na wataalamu wa mifugo kwa kuleta chanjo ya kideli kwa ajili ya kuku kwani itasaidia kukabiliana na ugonjwa wa kideli ambao umekuwa changamoto kubwa kwa Wafugaji wa kuku.
Mwakilishi wa Wafugaji kata ya Lwangwa Bi.Tulinagwe Stashoni ameiomba serikali zoezi la chanjo ya kideli liwe endelevu kwa sababu wafugaji wanateseka na wamekuwa wakipata hasara sana kutokana na ugonjwa wa kideli pia ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwakumbuka Wafugaji wa kuku.
Uzinduzi wa chanjo ya kideli cha kuku katika Halmashauri ya Busokelo ni hatua muhimu katika ukuzaji endelevu wa ufugaji wa kuku.kwa kuku walio salama ma wenye afya,uzinduzi huu unaimarisha jitihada za serikali katika kuhakikisha ufugaji unakuwa imara katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Lwangwa, Tukuyu
Anuani ya Posta: S. L. P. 2, Tukuyu
Simu: +255 737 205 318
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@busokelodc.go.tz
Hakimiliki ©2019 Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo. Haki zote zimehifadhiwa.