• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Busokelo District Council
Busokelo District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Busokelo District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Adminstration
    • Organization Structure
    • Departments
      • Adminstration and Human Resource
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Health
      • Water
      • Sanitation and Environment
      • Agriculture, Irrigation and Cooperatives
      • Livestock and Fisheries
      • Development and Social Walfare
      • Land and Natural Resouces
      • Construction, Fire and Works
    • Units
      • Internal Audit
      • Bee Keeping
      • Election
      • Legal
      • Ict
      • Procurement and Supplies
  • Investment Oppotunities
    • Tourism
    • Agricultural
    • Livestock
    • Fishing
    • Bee Keeping
    • Industries
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • Councilors list
    • Standing Committee
      • Finance Planning and Adminstration
      • Economy Works and Environment
      • Education Health and Water
      • CMAC
      • Ethics committee
    • Schedules
      • Councilors schedule meetings
      • Chairperson schedule
  • Projects
    • Planned projects
    • On going projects
    • Completed projects
  • Publications
    • Acts
    • Customer service contrct
    • Strategic plan
    • Reports
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery

IJUE MAMLAKA YA SERIKALI ZA MITAA TANZANIA

Posted on: November 5th, 2024

MFUMO WA SERIKALI ZA MITAA TANZANIA 


Malengo Mahsusi



Baada ya kujifunza mada hii utaweza:


  1. Kufafanua mfumo wa utendaji wa serikali za mitaa,
  2. Kueleza majukumu na kazi za Serikali za Mitaa,
  3. Kubainisha mahusiano kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa,
  4. Kutambua sheria zinazotawala uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa,
  5. Kubainisha umuhimu wa mahusiano bora baina ya watendaji na viongozi mbalimbali wakiwemo wa kisiasa ndani ya Mamlaka za serikali za mitaa.



1.2 Maana ya Serikali za Mitaa

Serikali za Mitaa hutafsiriwa kama vyombo vya wananchi ambavyo huundwa, huendeshwa, husimamiwa na kuwajibika kwa wananchi. Hapa nchini Tanzania vyombo hivi vimeanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 145 na 146 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sura ya 2 zinazobeba dhana ya ugatuzi wa madaraka. Yakupasa kuelewa kuwa Serikali za Mitaa ni sehemu ya serikali ambayo iko karibu zaidi na wananchi na inatoa huduma ambazo zinaendana na mahitaji ya wananchi husika katika eneo lao.

Angalizo



Tambua kuwa Serikali za Mitaa zinatokana na dhana ya ugatuaji wa madaraka kwa umma.


Dhana na madhumuni ya madaraka kwa umma ni kuwapatia wananchi uwezo na fursa ya kushiriki kikamilifu katika masuala ya siasa, uchumi na uendeshaji wa nchi yao chini ya Ibara ya 8 (1) (a) ya Katiba.

Swali la Tafakuri



Eleza dhana ya madaraka kwa umma katika undeshaji wa Serikali za Mitaa.



1.3 Historia ya Serikali za Mitaa

Baada ya kujifunza maana ya Serikali za Mitaa, kipengele hiki kinakueleza kuwa Serikali za Mitaa zimepitia katika vipindi vitatu ambavyo ni kabla ya ukoloni, wakati wa ukoloni na baada ya ukoloni.

1.3.1 Serikali za Mitaa Kabla ya Ukoloni

Mfumo wa Serikali za Mitaa umekuwepo tangu binadamu walipoanza kuishi pamoja ili kujilinda na wanyama au wavamizi. Kipindi hicho jamii ziliongozwa na watu waliokuwa wanaheshimika na wenye ushawishi. Baadhi ya jamii zilianzisha mabaraza ya wazee kwa ajili ya kujadili na kuamua masuala kuhusu usalama na ustawi wao. Kadiri jamii zilivyoendelea kukua, zilichagua machifu/watemi wa kuwaongoza wakisaidiana na mabaraza ya wazee.

1.3.2 Serikali za Mitaa Wakati wa Ukoloni

Katika kipindi hiki, nchi yetu ilitawaliwa na tawala mbili za kikoloni yaani Mjerumani na Muingereza. Kipindi cha utawala wa Mjerumani hapakuwa na juhudi mahsusi za kuanzisha Serikali za Mitaa kwani walitumia mfumo wa utawala wa moja kwa moja usioshirikisha wazawa.

Kipindi cha utawala wa Muingereza kulishuhudiwa juhudi za kuanzisha, kuendeleza na kudumisha mfumo wa Serikali za Mitaa. Sheria mbalimbali zilitungwa ikiwemo Sheria ya Mamlaka za Wazawa ya mwaka 1926 iliyowapa machifu mamlaka ya kiuongozi, kiutawala na kimahakama; Sheria ya Manispaa ya mwaka 1946 iliyoanzisha manispaa ya Dar es Salaam mwaka 1948; na Sheria ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1953 iliyoanzisha mfumo wa Serikali za Mitaa ambao kwa kiasi kikubwa ulirithiwa baada ya uhuru.

1.3.3 Serikali za Mitaa Baada ya Ukoloni

Serikali za Mitaa baada ya ukoloni zimepitia vipindi vikuu vinne ambavyo ni; miaka kumi ya kwanza ya uhuru, kipindi cha mfumo wa Madaraka Mikoani, urejeshwaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, na kipindi cha Maboresho ya Serikali za Mitaa.

Katika kipindi cha miaka kumi ya mwanzo wakati wa uhuru, serikali ya Tanganyika ilirithi sehemu kubwa ya mfumo wa Serikali za Mitaa wa utawala wa Muingereza lakini ilifuta Sheria ya Mamlaka za Wazawa ya mwaka 1926 ili kuimarisha umoja wa taifa changa la Tanganyika na kuanzisha rasmi Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Mwaka 1972, serikali ilifuta Mamlaka za Serikali za Mitaa na kuanzisha mfumo wa madaraka mikoani ambao ulilenga kupeleka mamlaka za serikali katika ngazi za msingi kuanzia ngazi ya Mkoa mpaka Vijiji. Mfumo huo ulishindwa kufikia adhma ya kuwashirikisha wananchi na kuboresha huduma kama ilivyotazamiwa.

Ni vema ufahamu kuwa kutokana na changamoto za mfumo wa Madaraka Mikoani ulioanzishwa katika aya iliyotangulia, serikali iliona umuhimu wa kurejesha mamlaka za Serikali za Mitaa mwaka 1982. Urejeshwaji huo ulienda sambamba na utungaji wa sheria mbalimbali za serikali za mitaa, ikiwa ni pamoja na marekebisho ya Katiba ya nchi ya mwaka 1984 ili kutambua mfumo wa serikali za mitaa nchini. Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya), Sura ya 287 na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Sura ya 288 zilitungwa ili kurejesha mfumo wa Serikali za Mitaa.

Baada ya kurejesha Mfumo wa Serikali za Mitaa, na kutokana na changamoto mbalimbali serikali iliamua kufanya maboresho ya serikali za Mitaa kupitia Sera ya Maboresho ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1998. Sera hiyo ililenga kuboresha maeneo manne yaliyojumuisha: Ugatuaji wa madaraka ya kisiasa, kifedha, kiutawala na maboresho ya mahusiano kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa, ili kuzipa Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM) uhuru na madaraka ya kutekeleza majukumu kwa ufanisi katika maeneo yao.

1.4 Sheria na Uhalali wa Serikali za Mitaa

Ni vema ukatambua kuwa, uhalali wa MSM unatokana na Ibara ya 145 na 146 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na unatokana na dhana ya kupeleka madaraka kwa umma. Hivyo, uundwaji, utendaji, maamuzi na uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa hufanyika kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria zilizotungwa na Bunge na miongozo mbalimbali. Rejea kielelezo Na. 1.1.

Announcements

  • TANGAZO LA KUITWA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA. December 09, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA AJIRA YA MKATABA October 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA AJIRA April 11, 2023
  • TANGAZO LA UKODISHAJI MAGHALA YA KUHIFADHIA KOKOA June 05, 2024
  • View All

Latest News

  • MHE. HOMERA AHIMIZA USHIRIKIANO WA WANANCHI NA SERIKALI UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO.

    June 11, 2025
  • KIDELI SASA BASI, CHANJO YA KUKU YA YAZINDULIWA RASMI BUSOKELO.

    June 09, 2025
  • MAFANIKIO SEKTA YA KILIMO HALMASHAURI YA BUSOKELO MWAKA 2024/2025.

    June 06, 2025
  • KAMPUNI YA UJENZI WA BARABARA YA CHINA ROADS AND BRIDGE CO-OPERATION YASAINI MKATABA WA KUWA MPANGAJI KATIKA MAKAMBI YA MBAMBO.

    May 29, 2025
  • View All

Video

Mkurugenzi atoa hamasa ya chakula kwa watoto mashuleni
More Videos

Quick Links

  • Watumishi Portal
  • Salary slip
  • Councilors list
  • Gallery

Related Links

  • President's Office, Public Service Management
  • TAMISEMI
  • e-Government Agency
  • President's Officia Website
  • Mbeya Regional Website
  • Public Service Recruitment Secretariet

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Lwangwa, Tukuyu

    Postal Address: S. L. P. 2, Tukuyu

    Telephone: +255 737 205 318

    Mobile:

    Email: ded@busokelodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 Busokelo DC . All rights reserved.