• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua ya Pepe |
Busokelo District Council
Busokelo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Usafishaji na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi na Zima moto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

IJUE MAMLAKA YA SERIKALI ZA MITAA TANZANIA

Imewekwa tarehe: November 5th, 2024

MFUMO WA SERIKALI ZA MITAA TANZANIA 


Malengo Mahsusi



Baada ya kujifunza mada hii utaweza:


  1. Kufafanua mfumo wa utendaji wa serikali za mitaa,
  2. Kueleza majukumu na kazi za Serikali za Mitaa,
  3. Kubainisha mahusiano kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa,
  4. Kutambua sheria zinazotawala uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa,
  5. Kubainisha umuhimu wa mahusiano bora baina ya watendaji na viongozi mbalimbali wakiwemo wa kisiasa ndani ya Mamlaka za serikali za mitaa.



1.2 Maana ya Serikali za Mitaa

Serikali za Mitaa hutafsiriwa kama vyombo vya wananchi ambavyo huundwa, huendeshwa, husimamiwa na kuwajibika kwa wananchi. Hapa nchini Tanzania vyombo hivi vimeanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 145 na 146 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sura ya 2 zinazobeba dhana ya ugatuzi wa madaraka. Yakupasa kuelewa kuwa Serikali za Mitaa ni sehemu ya serikali ambayo iko karibu zaidi na wananchi na inatoa huduma ambazo zinaendana na mahitaji ya wananchi husika katika eneo lao.

Angalizo



Tambua kuwa Serikali za Mitaa zinatokana na dhana ya ugatuaji wa madaraka kwa umma.


Dhana na madhumuni ya madaraka kwa umma ni kuwapatia wananchi uwezo na fursa ya kushiriki kikamilifu katika masuala ya siasa, uchumi na uendeshaji wa nchi yao chini ya Ibara ya 8 (1) (a) ya Katiba.

Swali la Tafakuri



Eleza dhana ya madaraka kwa umma katika undeshaji wa Serikali za Mitaa.



1.3 Historia ya Serikali za Mitaa

Baada ya kujifunza maana ya Serikali za Mitaa, kipengele hiki kinakueleza kuwa Serikali za Mitaa zimepitia katika vipindi vitatu ambavyo ni kabla ya ukoloni, wakati wa ukoloni na baada ya ukoloni.

1.3.1 Serikali za Mitaa Kabla ya Ukoloni

Mfumo wa Serikali za Mitaa umekuwepo tangu binadamu walipoanza kuishi pamoja ili kujilinda na wanyama au wavamizi. Kipindi hicho jamii ziliongozwa na watu waliokuwa wanaheshimika na wenye ushawishi. Baadhi ya jamii zilianzisha mabaraza ya wazee kwa ajili ya kujadili na kuamua masuala kuhusu usalama na ustawi wao. Kadiri jamii zilivyoendelea kukua, zilichagua machifu/watemi wa kuwaongoza wakisaidiana na mabaraza ya wazee.

1.3.2 Serikali za Mitaa Wakati wa Ukoloni

Katika kipindi hiki, nchi yetu ilitawaliwa na tawala mbili za kikoloni yaani Mjerumani na Muingereza. Kipindi cha utawala wa Mjerumani hapakuwa na juhudi mahsusi za kuanzisha Serikali za Mitaa kwani walitumia mfumo wa utawala wa moja kwa moja usioshirikisha wazawa.

Kipindi cha utawala wa Muingereza kulishuhudiwa juhudi za kuanzisha, kuendeleza na kudumisha mfumo wa Serikali za Mitaa. Sheria mbalimbali zilitungwa ikiwemo Sheria ya Mamlaka za Wazawa ya mwaka 1926 iliyowapa machifu mamlaka ya kiuongozi, kiutawala na kimahakama; Sheria ya Manispaa ya mwaka 1946 iliyoanzisha manispaa ya Dar es Salaam mwaka 1948; na Sheria ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1953 iliyoanzisha mfumo wa Serikali za Mitaa ambao kwa kiasi kikubwa ulirithiwa baada ya uhuru.

1.3.3 Serikali za Mitaa Baada ya Ukoloni

Serikali za Mitaa baada ya ukoloni zimepitia vipindi vikuu vinne ambavyo ni; miaka kumi ya kwanza ya uhuru, kipindi cha mfumo wa Madaraka Mikoani, urejeshwaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, na kipindi cha Maboresho ya Serikali za Mitaa.

Katika kipindi cha miaka kumi ya mwanzo wakati wa uhuru, serikali ya Tanganyika ilirithi sehemu kubwa ya mfumo wa Serikali za Mitaa wa utawala wa Muingereza lakini ilifuta Sheria ya Mamlaka za Wazawa ya mwaka 1926 ili kuimarisha umoja wa taifa changa la Tanganyika na kuanzisha rasmi Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Mwaka 1972, serikali ilifuta Mamlaka za Serikali za Mitaa na kuanzisha mfumo wa madaraka mikoani ambao ulilenga kupeleka mamlaka za serikali katika ngazi za msingi kuanzia ngazi ya Mkoa mpaka Vijiji. Mfumo huo ulishindwa kufikia adhma ya kuwashirikisha wananchi na kuboresha huduma kama ilivyotazamiwa.

Ni vema ufahamu kuwa kutokana na changamoto za mfumo wa Madaraka Mikoani ulioanzishwa katika aya iliyotangulia, serikali iliona umuhimu wa kurejesha mamlaka za Serikali za Mitaa mwaka 1982. Urejeshwaji huo ulienda sambamba na utungaji wa sheria mbalimbali za serikali za mitaa, ikiwa ni pamoja na marekebisho ya Katiba ya nchi ya mwaka 1984 ili kutambua mfumo wa serikali za mitaa nchini. Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya), Sura ya 287 na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Sura ya 288 zilitungwa ili kurejesha mfumo wa Serikali za Mitaa.

Baada ya kurejesha Mfumo wa Serikali za Mitaa, na kutokana na changamoto mbalimbali serikali iliamua kufanya maboresho ya serikali za Mitaa kupitia Sera ya Maboresho ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1998. Sera hiyo ililenga kuboresha maeneo manne yaliyojumuisha: Ugatuaji wa madaraka ya kisiasa, kifedha, kiutawala na maboresho ya mahusiano kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa, ili kuzipa Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM) uhuru na madaraka ya kutekeleza majukumu kwa ufanisi katika maeneo yao.

1.4 Sheria na Uhalali wa Serikali za Mitaa

Ni vema ukatambua kuwa, uhalali wa MSM unatokana na Ibara ya 145 na 146 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na unatokana na dhana ya kupeleka madaraka kwa umma. Hivyo, uundwaji, utendaji, maamuzi na uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa hufanyika kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria zilizotungwa na Bunge na miongozo mbalimbali. Rejea kielelezo Na. 1.1.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA. December 09, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA AJIRA YA MKATABA October 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA AJIRA April 11, 2023
  • TANGAZO LA UKODISHAJI MAGHALA YA KUHIFADHIA KOKOA June 05, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. HOMERA AHIMIZA USHIRIKIANO WA WANANCHI NA SERIKALI UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO.

    June 11, 2025
  • KIDELI SASA BASI, CHANJO YA KUKU YA YAZINDULIWA RASMI BUSOKELO.

    June 09, 2025
  • MAFANIKIO SEKTA YA KILIMO HALMASHAURI YA BUSOKELO MWAKA 2024/2025.

    June 06, 2025
  • KAMPUNI YA UJENZI WA BARABARA YA CHINA ROADS AND BRIDGE CO-OPERATION YASAINI MKATABA WA KUWA MPANGAJI KATIKA MAKAMBI YA MBAMBO.

    May 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Mkurugenzi atoa hamasa ya chakula kwa watoto mashuleni
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • Hati ya Mshahara
  • Orodha ya Madiwani
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Rais
  • Tovuti ya Mkoa wa Mbeya
  • Sekretarieti ya Ajira

Kipimo cha Wateja duniani

world map hits counter

Wateja waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Lwangwa, Tukuyu

    Anuani ya Posta: S. L. P. 2, Tukuyu

    Simu: +255 737 205 318

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@busokelodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2019 Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo. Haki zote zimehifadhiwa.