• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua ya Pepe |
Busokelo District Council
Busokelo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Usafishaji na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi na Zima moto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

CMT BUSOKELO YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, YAAGIZA MIRADI YOTE IKAMILIKE IFIKAPO 20/01/2026.

Imewekwa tarehe: January 15th, 2026


CMT – BUSOKELO YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, YAAGIZA MIRADI YOTE IKAMILIKE IFIKAPO 20/01/2026.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo (Wilaya ya Rungwe), Bw. Raphael Mputa, ameongoza Timu ya Menejimenti ya Halmashauri (CMT) kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata tofauti za Busokelo kwa lengo la kuhakikisha inatekelezwa kwa ubora, kwa wakati na kwa thamani halisi ya fedha. Zoezi hili la ukaguzi wa miradi limefanyika leo tarehe 15 Januari 2026.

Katika ukaguzi huo, Bw. Mputa amesisitiza kuwa miradi yote ikamilike ifikapo tarehe 20 Januari 2026 kama ilivyoagizwa na Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Mhe. Jaffar Haniu, katika ziara iliyopita, ili wananchi waanze kunufaika mapema na huduma bora za elimu, uchumi na utawala bora. Aidha, Timu ya Menejimenti ya Halmashauri (CMT) imehimiza usimamizi wa karibu wa miradi, utunzaji wa nyaraka na uwajibikaji katika kila hatua ya utekelezaji.

Miradi hii inalenga kuboresha huduma za elimu kwa watoto, kuongeza fursa za ajira na kipato kwa wananchi, kuwawezesha wanawake na vijana kiuchumi pamoja na kuimarisha miundombinu ya utawala, hivyo kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo.

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na matundu sita ya vyoo katika Shule ya Msingi Manambano, unaotekelezwa kwa fedha za BOOST zenye thamani ya shilingi milioni 70.1, ujenzi wa majengo ya Shule Mpya ya Msingi Lusanje – Mkonodo Mmoja, unaotekelezwa kwa fedha za BOOST zenye thamani ya shilingi milioni 329.5.

Miradi mingine ni pamoja na ujenzi wa madarasa matatu na matundu sita ya vyoo katika Shule ya Msingi Kandete, unaotekelezwa kwa fedha za BOOST zenye thamani ya shilingi milioni 88, ujenzi wa Shule Mpya ya Elimu ya Awali na Msingi Mwakaleli, unaotekelezwa kwa fedha za BOOST zenye thamani ya shilingi milioni 329.5,

Mradi wa Kikundi cha Wanawake Amka wa ufugaji wa ng’ombe wa maziwa, unaotekelezwa kwa mapato ya ndani ya Halmashauri yenye thamani ya shilingi  milioni 5.

Aidha, mradi wa ukamilishaji wa Nyumba ya Mkurugenzi wa Halmashauri, unaotekelezwa kwa fedha za Serikali Kuu zenye thamani ya shilingi milioni 70, pamoja na ukamilishaji wa Jengo la Utawala, unaotekelezwa kwa fedha za Serikali Kuu zenye thamani ya shilingi bilioni 1.

Miradi hiyo inatekelezwa kwa ushirikiano wa karibu kati ya Serikali na Wananchi, ambapo Serikali imetoa fedha kupitia miradi ya BOOST, Serikali Kuu na Mapato ya Ndani, huku wananchi wakichangia nguvu kazi, ulinzi wa miradi na ushirikiano wa kijamii ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora na maendeleo endelevu katika Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo.

Kwa ujumla, miradi yote iliyokaguliwa ina thamani ya shilingi 1,892,100,000, fedha ambazo zinaonesha dhamira ya dhati ya Serikali kwa kushirikiana na wananchi katika kuboresha elimu, uchumi na utawala bora kwa maendeleo ya Busokelo.






Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA. December 09, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA AJIRA YA MKATABA October 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA AJIRA April 11, 2023
  • TANGAZO LA UKODISHAJI MAGHALA YA KUHIFADHIA KOKOA June 05, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • CMT BUSOKELO YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, YAAGIZA MIRADI YOTE IKAMILIKE IFIKAPO 20/01/2026.

    January 15, 2026
  • SHILINGI BILIONI 32.9 ZAIDHINISHWA BAJETI YA HALMASHAURI MWAKA WA FEDHA 2026/2027.

    January 14, 2026
  • MIRADI YA MAENDELEO YENYE JUMLA YA THAMANI YA SHILINGI BILIONI 6.6 YAKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA BUSOKELO.

    October 10, 2025
  • RC MALISA AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA BUSOKELO.

    September 24, 2025
  • Angalia zote

Video

Mkurugenzi atoa hamasa ya chakula kwa watoto mashuleni
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • Hati ya Mshahara
  • Orodha ya Madiwani
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Rais
  • Tovuti ya Mkoa wa Mbeya
  • Sekretarieti ya Ajira

Kipimo cha Wateja duniani

world map hits counter

Wateja waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Lwangwa, Tukuyu

    Anuani ya Posta: S. L. P. 2, Tukuyu

    Simu: +255 737 205 318

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@busokelodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2019 Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo. Haki zote zimehifadhiwa.