• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua ya Pepe |
Busokelo District Council
Busokelo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Usafishaji na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi na Zima moto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

ELIMU KUHUSU UMUHIMU WA BIMA YA AFYA YA iCHF ITOLEWE ZAIDI KWA WANANCHI WA BOSOKELO.

Imewekwa tarehe: August 2nd, 2023

ELIMU KUHUSU  UMUHIMU  WA BIMA YA AFYA YA  iCHF ITOLEWE ZAIDI KWA WANANCHI WA BOSOKELO.

NA PETER TUNGU.

Katika Kuboresha utowaji wa huduma za afya kwa wananchi wa Busokelo, Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo Mkoa wa Mbeya  limewaagiza Watumishi wa Idara  ya afya  Busokelo waendelee kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa Bima ya Afya iliyo rahisishwa iCHF ili kuwahamasisha wananchi wengi kujiunga katika bima ya iCHF kwaajili ya kupatiwa matibabu katika vituo vya kutoelwa huduma za afya vinavyo patikana katika Halmashauri ya Busokelo.

Hayo yameelezwa  katika Kikao cha robo ya nne 2022/2023 cha Baraza la Madiwani  Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo kilichofanyika leo tarahe 02/08/2023 katika ukumbi mpya wa mikutano wa Halmashauri hiyo kikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe.Anyosisye Njobelo na kuhudhuria na wajumbe Waheshimiwa madiwani wa kata na Viti maalamu, na wataalamu kutoka Halmashauri ya wilaya Busokelo akichangia hoja kuhusu kamati ya fedha na mipango katika suala la ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ,Diwani wa viti maalum CCM Mhe.  Essah J.Msiku  aliwashauri  wataalamu wa idara ya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo waendelee zaidi kutoa  eilimu kwa Wananchi wa Busokelo hasa maeneo ya vijijini kuhusu umuhimu wa Bima  ya afya ya iCHF ili kupata wanachama wengi zaidi katika mfuko huo na  wananchi waweze kupata huduma za afya kwa urahisi hasa waishio katika maeneo ya vijijini.  “ukiangalia kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kwenye chanzo cheti cha iCHF tulikuwa na aslimia 81% lakini kwa mwaka fedha 2022/2023 tumefikia asilimia 91.29% nitume nafasi hii kumpongeza Mkurgenzi na kamati kwa usimamizi mzuri, nipende kushauri kuongeza bidii na juhudi kwa wananchi ili waendelee kujiunga na ili tuweze kuongeza mapato na wananchi waweze kufaidika nah ii huduma” amesema Mhe. Msiku.

Bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa  iCHF ni Bima ya Afya iliyoanzishwa na serikali ya Tanzania chini ya Ofisi ya  Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tamisemi kwa kushirikiana na Wizara ya Afya amabapo huduma za matibabu hutolewa kwa mwanachama  mwenye kadi ya CHF kuanzia Zahanati, Kituo cha Afya , Hospitali  za Wilaya na Mikoa kwa nchi nzima.

Aidha katika hatua nyingine Diwani wa Kata ya Mpata Mhe.Mekara O.Mwangombola alihoji ni lini serikali  itahakikisha kila Kijiji kinakuwa na Zahanati ikwemo Kijiji cha Ipagika kilichopo katika Halmahsuari ya Busokelo Mkoa wa Mbeya.

Akijibu swali hilo Mwenyikiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo Mhe. Anyosisye Njobelo alisema kuwa jukumu la kujenga zahanati ni jukumu la wanakijiji na Serikali huwaunga mkono wanakijiji katika hatua hiyo.  “Mwongozo unaelekeza kuwa kila kata iwe na kituo cha afya na kila kijiji kiwe na Zahanati, sasa kuanziasha zahanati siyo  serikali kinaanzisha kijiji ndiyo serikali unawaunga mkono, sasa wana Ipagika kawaambie Serikali inataka wawe na mahali pakujenga,watenge eneo lipimwe  litambulike kisheria  halafu pale ndiyo waanzishe zahanati na serikali itwaaunga mkono” alisema Mhe.Njobelo, 

Naye katibu wa Baraza la Madiwani ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo Mhe.Loema I.Peter alisema kuwa  katika utekelezaji ujenzi miradi ya afya, Halmashauri hutenga fedha kwaajili ya ukamilishaji maboma ambayo wananchi wameyajenga  “Katika bajeti ya Halmashauri huwa tunatengea bajeti ya maboma ambayo wananchi wamekwisha jenga, Serikali  inatengea bajeti kwaajili ya kumalizia maboma hayo  na tumefanya hivyo kwa miaka kadhaa,ni maboma kadhaa yameshaletewa fedha katika upande wa afya na elimu pia, mfano halisi mwaka uliyopita tulipokea  ukamilishaji wa maboma nane(8) ya zahanati ,kila boma lilitengewa  milioni 75 ,na utaratibu ni uleule Mheshimiwa Mwenyekiti kwa hiyo wananchi wao waendelee kujenga maboma kwa wingi, kila  tutakapo andaa bajeti tutakuwa tunatenga kwajili ya  kukamilisha hayo maboma’’ alisema Mhe. Loema.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA. December 09, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA AJIRA YA MKATABA October 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA AJIRA April 11, 2023
  • TANGAZO LA UKODISHAJI MAGHALA YA KUHIFADHIA KOKOA June 05, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • KAMPUNI YA UJENZI WA BARABARA YA CHINA ROADS AND BRIDGE CO-OPERATION YASAINI MKATABA WA KUWA MPANGAJI KATIKA MAKAMBI YA MBAMBO.

    May 29, 2025
  • ELIMU YAHATUA ZA KUWASILISHA MALALAMIKO KWA WATUMIAJI WA TAASISI ZA KIFEDHA.

    March 21, 2025
  • WANANCHI KATA YA LUFILYO WAFIKIWA NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

    March 10, 2025
  • DC HANIU ATEMBELEA KALAKANA ZILIZOPO CHUO CHA VETA BUSOKELO

    March 01, 2025
  • Angalia zote

Video

Mkurugenzi atoa hamasa ya chakula kwa watoto mashuleni
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • Hati ya Mshahara
  • Orodha ya Madiwani
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Rais
  • Tovuti ya Mkoa wa Mbeya
  • Sekretarieti ya Ajira

Kipimo cha Wateja duniani

world map hits counter

Wateja waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Lwangwa, Tukuyu

    Anuani ya Posta: S. L. P. 2, Tukuyu

    Simu: +255 737 205 318

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@busokelodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2019 Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo. Haki zote zimehifadhiwa.