• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua ya Pepe |
Busokelo District Council
Busokelo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Usafishaji na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi na Zima moto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKIANENI NA WATENDAJI WA VIJIJI KUWAHUDUMIA WANANCHI.

Imewekwa tarehe: December 11th, 2024

SHIRIKIANENI NA WATENDAJI WA VIJIJI KUWAHUDUMIA WANANCHI.


Viongozi wa Serikali za Vijiji wametakiwa kufunya kazi kwa weledi, uzalendo na  moyo wa kujituma kwa kushirikiana na Watendaji wa vijiji ili kuwatumikia Wananchi kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla.

Wito huo umetolewa leo 11/12/2024 na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo Mhe.Anyosisye Njobelo wakatika akifungua Mafunzo ya Uongozi na Utumishi kwa Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Wajumbe wa Halmashauri za vijiji katika Kata za Mpombo, Kandete, Isange na Luteba.

Zaidi ya Viongozi 400 wa Serikali za Vijiji wakiwemo Wenyeviti wa Vijiji,Wenyeviti wa Vitongoji na Wajumbe wa Halmashaurui za vijiji kutoka ukanda wa Mwakaleli wamepatiwa mafunzo ya Uongozi katika bwalo la Mwakaleli Sekondari ili kuwajengea uwezo wa namna ya kuwatumikia Wananchi katika nafasi mbalimbali za uongozi walizochaguliwa  katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024.

‘’Baada ya kuchaguliwa na Wananchi wenu, mlikula kiapo cha utii, Mafunzo haya muyatumie vizuri ili mkawatumikie Wananchi katika vijiji venu, kuweni wazalendo, mkashirikiane na Watendaji wa vijiji  kutatua kero zote katika maeneo yenu kwa haki, usawa na kujituma ili muwaletee maendeleo Wananchi waliyo wachagua” alisema Mhe.Njobelo.

Kwa Upande wake Afisa Utumishi Halmshauri ya Wilaya ya Busokelo Bw.Fredrick Kweka aliwasilisha mada kuhusu Majumuku ya Wenyeviti wa vijiji, Wenyeviti wa vitongoji na Wajumbe wa Halmashauri za vijiji  pamoja na majukumu ya Mtendaji wa kijiji na wajibu wa Serikali za vijiji kwa Wananchi ili kuongeza uelewa  katika utekelezaji majukumu kwa viongozi hao.

Katika Hatua nyingine Afisa Mapato Halmashauri ya Busokelo Bi.Abella Ndamugoba aliwajengea zaidi uwezo Viongozi wa Serikali za vijiji kuhusu madhara ya utoroshaji wa mapato na umuhimu wa kusimamia ukusanyaji wa maopato katika vijiji huku akiwataka kutowafumbia macho wale wote wanao shiriki katika utoroshaji mapato kwenye vijiji kwani wanadhoofisha maendeleo ya kijiji husika.

Aidha Bw.Elia Msukwa Afisa Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo aliwaeleza Viongozi hao namna ambavyo migorororo ya ardhi inavyokwamisha shughuli za maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na kijiji kwa ujmla huku akiwataka kutokuwa chanzo cha migogoro ya ardhi na badala yake waishauri jamii kufikia mwafaka mzuri katika utatuzi wa migogoro ya ardhi kwa kuzingatia sheria kanuni na miongozo iliyowekwa.

Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo, Idara ya Utawala na Rasilimali Watu imeratibu mafunzo ya uongozi na utumishi kwa viongozi wote Serikali za Mitaa waliyongia madarakani  mwaka 2024 katika kata zote 13 za Busokelo ili kuwajengea uwezo wa kutwekeleza majukumu yao.

Tayari Viongozi wa vijiji kutoka kataza Isange, Kandete, Luteba,Mpata, Kabula, Lwangwa na Lupata wameshapatiwa mafunzo ya Uongozi , zoezi la utoaji mafunzo hayo linaendelea katika ukanda wa Lufilyo.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA. December 09, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA AJIRA YA MKATABA October 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA AJIRA April 11, 2023
  • TANGAZO LA UKODISHAJI MAGHALA YA KUHIFADHIA KOKOA June 05, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • KAMPUNI YA UJENZI WA BARABARA YA CHINA ROADS AND BRIDGE CO-OPERATION YASAINI MKATABA WA KUWA MPANGAJI KATIKA MAKAMBI YA MBAMBO.

    May 29, 2025
  • ELIMU YAHATUA ZA KUWASILISHA MALALAMIKO KWA WATUMIAJI WA TAASISI ZA KIFEDHA.

    March 21, 2025
  • WANANCHI KATA YA LUFILYO WAFIKIWA NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

    March 10, 2025
  • DC HANIU ATEMBELEA KALAKANA ZILIZOPO CHUO CHA VETA BUSOKELO

    March 01, 2025
  • Angalia zote

Video

Mkurugenzi atoa hamasa ya chakula kwa watoto mashuleni
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • Hati ya Mshahara
  • Orodha ya Madiwani
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Rais
  • Tovuti ya Mkoa wa Mbeya
  • Sekretarieti ya Ajira

Kipimo cha Wateja duniani

world map hits counter

Wateja waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Lwangwa, Tukuyu

    Anuani ya Posta: S. L. P. 2, Tukuyu

    Simu: +255 737 205 318

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@busokelodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2019 Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo. Haki zote zimehifadhiwa.