• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua ya Pepe |
Busokelo District Council
Busokelo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Usafishaji na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi na Zima moto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

UZINDUZI ZAHANATI YA SELYA

Imewekwa tarehe: June 27th, 2024

MHE.HANIU AZINDUA ZAHANATI MPYA YA KIJIJI CHA ITETE.


Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Mhe. Jaffar Haniu amezindua rasmi huduma za matibabu katika zahanati mpya ya Selya katika Kata ya Itete.

Uzinduzi huo umefanyika leo 27/06/2024 katika kijiji cha Selya Kata ya Itete Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo.

Akizungumza na Wananchi wa Itete mara baada ya kukagua miundombinu ya zahanati hiyo pamoja vifaa tiba vilivyopo katika zahanati hiyo mpya, Mhe.Haniu amesema kuwa  Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan inahakikisha Wananchi wake katika maeneo yote nchini wanapata huduma bora za matibabu  katika maeneo yao ya karibu.

"Wito wangu kwenu, ninaomba tuitunze zahanati hii, hii ni ya kwetu ni nguvu zetu na ujenzi tulianza wenyewe na Serikali yetu ilituongezea  fedha za ukamilishaji vifaa tiba pamoja na Wataalamu, Serikali ya Awamu ya Sita inahakikisha Wananchi wake wanapata huduma bora za matibabu katika maeneo ya karibu ili kuondoa adha ya kusafiri umbali mrefu wa kufuata huduma za matibabu" Alisema Mhe. Haniu.

Aidha Mhe.Haniu amewataka Wananchi wa Itete kuitunza miundombinu ya Zahanati hiyo ili idumu  na akasisitiza kuendelezwe ushirikiano baina ya Wananchi na Wataalamu walipo katika zahanati hiyo.

Katika hatua nyingine Mhe. Haniu amemshukuru Mkurungenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo pamoja na Diwani wa Kata ya Itete na Wananchi wote kwa kushiriki kikamilifu katika usimamizi  wa miradi na kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi .

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo Bi.Loema Peter ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kutenga kiasi cha fedha shilingi Milioni 85 kwaajili ya Ukamilishaji wa Zahanati  hiyo, pia ameishukuru Kamati ya Ujenzi, Wananchi wa Selya na Mheshimiwa Diwani wa Kata ya Itete kwa kushirikiana tangu hatua za awali hadi kukamilika kwa zahanati hiyo.

Diwani wa Kata ya Itete Mhe.Gwandege M.Mwakigemo, Ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwezesha upatikanaji wa huduma muhimu za jamii kwa Wanakijiji wa Selya.


Ujenzi wa zahanati mpya ya Selya umegharimu shilingi Milioni 85 kutoka Serikali kuu, shilingi milioni 22 ikiwa ni nguvu za Wananchi na shilingi milioni 3 kutoka mfuko wa Jimbo.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA. December 09, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA AJIRA YA MKATABA October 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA AJIRA April 11, 2023
  • TANGAZO LA UKODISHAJI MAGHALA YA KUHIFADHIA KOKOA June 05, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • ELIMU YAHATUA ZA KUWASILISHA MALALAMIKO KWA WATUMIAJI WA TAASISI ZA KIFEDHA.

    March 21, 2025
  • WANANCHI KATA YA LUFILYO WAFIKIWA NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

    March 10, 2025
  • DC HANIU ATEMBELEA KALAKANA ZILIZOPO CHUO CHA VETA BUSOKELO

    March 01, 2025
  • WADAU WA VYAMA VYA SIASA BUSOKELO KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.

    December 21, 2024
  • Angalia zote

Video

Mkurugenzi atoa hamasa ya chakula kwa watoto mashuleni
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • Hati ya Mshahara
  • Orodha ya Madiwani
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Rais
  • Tovuti ya Mkoa wa Mbeya
  • Sekretarieti ya Ajira

Kipimo cha Wateja duniani

world map hits counter

Wateja waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Lwangwa, Tukuyu

    Anuani ya Posta: S. L. P. 2, Tukuyu

    Simu: +255 737 205 318

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@busokelodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2019 Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo. Haki zote zimehifadhiwa.