• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua ya Pepe |
Busokelo District Council
Busokelo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Usafishaji na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi na Zima moto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WADAU WA VYAMA VYA SIASA BUSOKELO KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.

Imewekwa tarehe: December 21st, 2024

WADAU WA VYAMA VYA SIASA BUSOKELO KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.

Afisa Mwandikishaji Jimbo la Busokelo Wakili.Peter Salama amewataka Wadau vya vyama vya siasa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo kwenda kuwahamasisha Wananchi wa Busokelo kujitokeza kushiriki zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura kuanzia 27/12/2024 hadi 02/01/2025.

Wakili Salama ametoa wito huo leo 21/12/2024 kwenye ukumbi wa Halmashauri  katika kikao maalaumu na Wadau wa Vyama vya siasa, viongozi wa madhehebu ya dini, Wawakilishi wa Wafanyabiashara  viongozi wa vyama vya michezo na wawakilishi wa Machifu kutoka Busokelo.

Akifungua Mkutano huo, Wakili Salama amesema kuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi INEC inafanya kazi kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali muhimu wakiwemo viongozi wa dini, viongozi vya vya siasa, Machifu, Wanamichezo na makundi yote ya vijana na Wazee kwa lengo la kuhamasisha jamii ijitokeze kushiriki zoezi la Uboreshi Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

“Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi inatambua mchango wenu, ninyi ni Viongozi mnaoishi na watu hao katika jamii zetu na mnazungumza na Wananchi moja kwa moja kupitia nyumba za ibada, Majukwaa ya siasa michezo , Biashara na shughuli za utamaduni, kila mmoja atumie nafasi yake kuwahamasisha Wananchi kwenda kuboresha taarifa zao pindi uboreshaji utakapoanza’’ Alismea Wakili Peter Salama

Aidha Wakili Salama amesema kuwa Mawakala wa vyama vya siasa wataruhusiwa kuwepo katika vituo vya uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kama Waangalizi wa vyama vyao na wao ndiyo wanaowafahamu Wapiga kura wao katika eneo husika na hivyo hawaturuhusiwa kuingilia majukumu ya Maafisa Waandikishaji katika vituo, badala yake watatimiza majukumu yao ya uwakala kwa kuzingatia sheria na miongozo katika kutekeleza zoezi hili.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 17 (1) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Na. 1 ya Mwaka 2024, Chama cha Siasa chenye usajili wa kudumu kinaweza kumteua mtu mmoja katika kila kituo cha uandikishaji kuwa Wakala wa Uandikishaji wa Wapiga Kura.

  1. Kufuatilia zoezi la uboreshaji na kutazama kama linazingatia Sheria, Kanuni na Maelekezo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.
  2. Kushirikiana na Waandishi Wasaidizi kutambua wakazi wa eneo hilo na kutoa taarifa juu ya watu wasio na sifa.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 16 (5) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Na. 1 ya Mwaka 2024, Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utakuwa mara mbili kati ya kipindi kinachoanza mara baada ya uchaguzi mkuu na kabla ya siku ya uteuzi. Wanaohusika katika zoezi hili ni wananchi ambao: -

  1. Wametimiza umri wa miaka 18 na kuendelea ambao hawakuandikishwa hapo awali;
  2. Watakaotimiza miaka 18 kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025;
  3. Waliojiandikisha awali na wamehama Kata au Jimbo moja kwenda jingine;
  4. Waliopoteza sifa mfano wale waliofariki kuondolewa katika Daftari;Wenye taarifa zilizokosewa wakati wa uandikishaji; na
  5. Waliopoteza au kadi zao kuharibika.
  6. Waliopoteza  au kazi zao kuharibika





Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA. December 09, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA AJIRA YA MKATABA October 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA AJIRA April 11, 2023
  • TANGAZO LA UKODISHAJI MAGHALA YA KUHIFADHIA KOKOA June 05, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • ELIMU YAHATUA ZA KUWASILISHA MALALAMIKO KWA WATUMIAJI WA TAASISI ZA KIFEDHA.

    March 21, 2025
  • WANANCHI KATA YA LUFILYO WAFIKIWA NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

    March 10, 2025
  • DC HANIU ATEMBELEA KALAKANA ZILIZOPO CHUO CHA VETA BUSOKELO

    March 01, 2025
  • WADAU WA VYAMA VYA SIASA BUSOKELO KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.

    December 21, 2024
  • Angalia zote

Video

Mkurugenzi atoa hamasa ya chakula kwa watoto mashuleni
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • Hati ya Mshahara
  • Orodha ya Madiwani
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Rais
  • Tovuti ya Mkoa wa Mbeya
  • Sekretarieti ya Ajira

Kipimo cha Wateja duniani

world map hits counter

Wateja waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Lwangwa, Tukuyu

    Anuani ya Posta: S. L. P. 2, Tukuyu

    Simu: +255 737 205 318

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@busokelodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2019 Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo. Haki zote zimehifadhiwa.