• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua ya Pepe |
Busokelo District Council
Busokelo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Usafishaji na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi na Zima moto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Elimu Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WALIO KATISHA MASOMO KUTOKANA KUPATA UJAUZITO WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUWAPA NAFASI YA KUREJA SHULENI KUENDELEA NA MASOMO.

Imewekwa tarehe: September 26th, 2023

WALIO KATISHA MASOMO KUTOKANA KUPATA UJAUZITO WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUWAPA NAFASI YA KUREJA SHULENI KUENDELEA NA MASOMO.


Wanafunzi wa kike waliokatisha masomo yao ya elimu ya sekondari kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupata ujazito, wamemshukuru Rais Dk.Samia  Suluhu Hassan kwa kuwapatia nafasi ya kurudi shuleni kuendelea na masomo ya Elmu ya sekondari.


Hayo yamejiri  26/09/2023 Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya, katika kituo cha Mafunzo Elimj kwa watu wazima mradi  wa SEQUIP shule ya Sekonadari Kiwira ambapo Afisa Elimu Mkoa wa Mbeya, Maafisa Elimu ya watu wazima na Wenyeviti wa Kamati huduma ya Jamii katika Halmashauri 7 za Mkoa wa Mbeya walifika   tembelea kituo cha SEQUIP kiwira  katika maadhimisho ya Juma la Elimu ya watu wazima.


Jumla ya wanafunzi wa kike 43 wanaendelea na masomo yao ya sekondari wakiwa ni miongoni wanafunzi waliyo katisha masomo yao hapo awali kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupata ujazito wakiwa masomoni.

Irene Isac Joseph ni miongoni mwa Wanafunzi wanaoendelea na masomo ya sekondari katika kituo cha SEQUIP Kiwira, anaeleza kwamba vishawishi vilimpelekea kushindwa  kuendelea na  masomo yake ya sekondari baada ya kubeba ujauzito.  " Sisi watoto wa kike tuna kabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo vishawishi vya kidunia, usipokuwa makini ni rahisi sana kushawishika, mimi nilibeba ujauzito hali iliyopekea kuacha masomo, ndoto yangu ilikuwa kuja kuwa Daktari lakini niliona siwezi ifikia baada ya kuacha masomo, lakini nina mshukuru sana Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia nafasi hii turudi shuleni kuendelea na masomo, ninaamini ndoto yangu ya kuwa Daktari itamia" alisema Irene.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo ambaye  ni Diwani wa Kata ya Ipagika, Mh.Mekara O.Mwang'ombola  alisema kuwa ni lazima sasa jamii ihamasike kwa ujumla kuwaibua watoto wote waliyokatisha masomo yao hapo awali kutokana na changamoto za ujauzito na sababu zingine waingizwe katika mpango wa SEQUIP na mafunzo ya Elimu ya vitendo kwa watu wazima  ili wapate elimu na maarifa yatayowasidia kufikia  ndoto zao.


Mkoa wa Mbeya una jumla ya vituo 12 vinayohudumia watoto wa kike waliyo katisha masomo yao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo hali duni ya kimaisha, ujauzito, utoro na Ugonjwa.


Kituo cha SEQUIP-AEP Kiwira Sekondari kipo kijiji cha Ilundo, Kata ya Kiwira Wilayani Rungwe, Mkoa wa Mbeya kilanza rasmi 18/02/2022 baada ya Rais Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kuamua kuwarejesha shuleni  Watoto wenye umri kuanzia miaka 13-21 waliyokatiza masomo yao kutokana na sababu mbalimbali ikwemo utoro, ujauzito, ugonjwa na hali duni ya maisha.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA. December 09, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA AJIRA YA MKATABA October 20, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA AJIRA April 11, 2023
  • TANGAZO LA UKODISHAJI MAGHALA YA KUHIFADHIA KOKOA June 05, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • KAMPUNI YA UJENZI WA BARABARA YA CHINA ROADS AND BRIDGE CO-OPERATION YASAINI MKATABA WA KUWA MPANGAJI KATIKA MAKAMBI YA MBAMBO.

    May 29, 2025
  • ELIMU YAHATUA ZA KUWASILISHA MALALAMIKO KWA WATUMIAJI WA TAASISI ZA KIFEDHA.

    March 21, 2025
  • WANANCHI KATA YA LUFILYO WAFIKIWA NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

    March 10, 2025
  • DC HANIU ATEMBELEA KALAKANA ZILIZOPO CHUO CHA VETA BUSOKELO

    March 01, 2025
  • Angalia zote

Video

Mkurugenzi atoa hamasa ya chakula kwa watoto mashuleni
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • Hati ya Mshahara
  • Orodha ya Madiwani
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Rais
  • Tovuti ya Mkoa wa Mbeya
  • Sekretarieti ya Ajira

Kipimo cha Wateja duniani

world map hits counter

Wateja waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Lwangwa, Tukuyu

    Anuani ya Posta: S. L. P. 2, Tukuyu

    Simu: +255 737 205 318

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@busokelodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2019 Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo. Haki zote zimehifadhiwa.